Fafanua nadharia zozote tatu zitakazotumiwa na mwalimu wa sekondari kufunzia lugha ya pili.

 

1.      Fafanua nadharia zozote tatu zitakazotumiwa na mwalimu wa sekondari kufunzia lugha ya pili. 

                              i.)            MBINU YA USOMAJI.

Mbinu hii inatumika kufundishia wanafunzi wanao jifunza lugha ya pili na ambapo hawatarajiwi kutoka nje ya nchi ambapo lugha hiyo inatumika. Lengo lake ni kuendeleza uwezo wa wanafunzi la kusoma lugha ile. Vipengele vinavyofundishwa ni vile vya usomaji.

 

                            ii.)            NADHARI YA MWALIMU ALIYE KIMYA.

Katika mbinu hii, mwalimu anatakiwa kuwa kimyakwa muda mwingi darasani ilhali mwanafunzi anatakikana kushirikishwa kuzungumza au kuandika kwa wingi.

Mbinu hii imetengenezwa kwa misingi ifuatayo:

a)      Ujifunzaji wa lugha ya pili unafanikishwa na vifaa halisi vya ufundishaji( vitu ambavyo vanaweza kuonekana na kushikika)

b)      Kwamba ujifunzaji wa lugha ya pili unafanikiwa ikiwa mwanafunzi anajigundulia mambo kwa ubunifu wake badala ya kurudiarudia na kukumbuka anachojifunza.

c)      Ufunzaji unafanikishwa kwa kushirikisha mwanafunzi kwa kile anachojifunza. Inashikilia kwa wanafunzi ni watendaji na siyo wasikivu tu.

 

                          iii.)            NADHARIA YA UFUNDISHAJI VITENDO

Nadharia ya ufundishaji kwa vitendo hudhamiria kufundisha lugha kwa matumizi ya vitendo. Wafuasi wa lugha hii huamini wanafunzi hujifunza lugha ya pili vizuri katika mazingira na hali ambayo haina wasiwasi.

Husaidia kuhitimisha  wanafunzi wanaoweza kuwasiliana bila vikwazo kwa sababu.

a.       Ufundishaji wa lugha ya pili wapaswa kusisitiza maana na wala siyo miundo.

b.      Matumizi ya vitendo amri ni muhimu katika ufundishaji wa lugha ya pili.

c.       Mwanafunzi anaweza kujifunza vipande viwili vikubwa kuliko sentensi.

d.      Wanafunzi husikiza na kujibu kwa vitendo.

e.       Usikilizaji ukiimarika uzungumzaji huimarika pia.

2.      Eleza umuhimu wa safu mbalimbali za ratiba 

Ratiba ni orodha ya mpangilio wa namna mambo yatakavyofuatana katika shughuli Fulani. Lengo lake ni kuhakikisha wakati unatumiwa vizuri ili mambo Fulani yasije yakakosa kutendwa kutokana na upungufu wa wakati.

Ratiba hutumiwa katika mazishi, hafla, tamasha na kwa masomo.

Ratiba humwezesha mwalimu kuhitimisha silabasi kwa muda uliopendekezwa.

Humwezesha mwalimu kuamua namna  ya kuhusisha mambo yanayohusiana na na kuamua mambo ya kusisitiza.

Humwezesha mwalimu kupanga ufundishaji wake ili ulingane nan a ugumu wa mambo au ulingane na kiwango cha lugha ya mwanafunzi na mpango wa mwalimu wa kutahini.

Ratiba humwezesha mwalimu kufikiria na kuandaa vielezo na vifaa mwafaka.

Safu mbalimabali za ratiba na umuhimu ufuatao.

-        Husaidia kutaja shughuli yenyewe husika kwa mfano siku ya zawadi au somo lenyewe.

-        Tarehe husaidia kuonyesha ni lini shughuli hiyo hufanyika.

-        Mahali husaidia kueleza mahali ambapo shughuli hiyo itafanyikia kwa mfano katika uwanja wa mchezo wa Tingolo au  darasa Fulani.

-        Muda husaidia kuonyesha saa ambazo tukio limepangiwa kuanza na kukamilika.

-        Wahusika husaidia kutaja watu waliopewa wajibu wa kutekeleza jambo Fulani kwa mfano mwalimu huwa na shughuli za kutekeleza na wanafunzi pia huwa na shughuli tofauti za kutekeleza.

-        Wiki husaidia mwalimu kujua ni juma lipi la muhula na kutekeleza wajibu wake ili kukamilisha kazi zake kwa wakati unaofaa.

-         Ratiba huwa na kupindi ambacho husaidia mwalimu kujua anashughulikia kipindi kipi kwa juma hilo lililotajwa.

-        Maoni  husaidia kufafanua jinsi shughuli ilivyoendelea kama ilikuwa ya ufanisi au la.

Comments

Popular posts from this blog

NI SABABU ZIPI ZINAZOFANYA MZUNGUMZAJI WA LUGHA KUFANYA MAKOSA YA KISARUFI NA KIMATAMSHI NA KIMANTIKI KATIKA LUGHA?

Methali, Vitendawili, nahau, misemo,

NADHARIA ZINAZOELEZEA CHIMBUKO LA FASIHI SIMULIZI/MASIMULIZI