Fafanua nadharia zozote tatu zitakazotumiwa na mwalimu wa sekondari kufunzia lugha ya pili.

 

Fafanua nadharia zozote tatu zitakazotumiwa na mwalimu wa sekondari kufunzia lugha ya pili. 

Kunazo nadharia (mikondo) za ufundishaji wa lugha ya pili  ambazo zimewahi kuathiri, na ambazo mpaka sasa zinaathiri, ufundishaji wa lugha ya pili. Nadharia hizo ni nyingi.

a) Nadharia ya ufundishaji wa moja kwa moja

Nadharia hii ilitumika sana Ulaya mwishoni mwa karne ya 19 na mwanzoni mwa karne ya 20. Nadharia hii ilisisitiza sana ufundishaji wa lugha ya pili kwa kuitumia lugha iyo hiyo. Iliwakataza walimu kutumia tafsiri ya aina yoyote katika ufundishaji wao. Katika nadharia hii, ilikuwa ni marufuku kutumia lugha ya mama katika ufundishaji wa lugha ya pili. Waasisi wa nadharia hii waliamini kuwa watu wanaweza kujifunza lugha ya pili namna wanavyo jifunza lugha ya kwanza, pasi na tafsiri au matumizi ya lugha nyingine yoyote. Kwao. Ujinzaji wa lugha ya pili ulikuwa ni sawa na kuzifuata nyayo za lugha ya kwanza ambapo yule anayejifunza huingiliana moja kwa moja na lugha anayojifunza bila tafsiri.

Nadharia ya ufundishaji wa moja kwa moja haikuhimiza uchambuzi wa sarufi au maelezo ya kisarufi kwa wanafunzi. Kwa mujibu wa nadharia hii, walimu walishauriwa kutotaja maneno kama’Nomino’, ‘Kitenzi’ na ‘Kivumishi’. Baada ya ufundishaji uliofanywa kwa uingizaji, na maonyesho ya vitu, kwa mfano, picha au vifaa vingine, wanafunzi walitakiwa kuzing’amua wenyeye sheria na kanuni za kisarufi. Wanadharia hii waliamini kuwa lugha hufunzika vizuri kwa kuitumia darasani na wala siyo kuichambua kisarufi.

Kwa mujibu wa nadharia hii, walimu walitakiwa kufundisha mazungumzo pamoja na ufahamu wa kusikiza. Mbinu ya maswali na majibu ilipendekezwa katika ufundishaji wa mazungumzo ambayo yalithaminiwa sana. Mwalimu aliuliza maswali nao wanafunzi waliyajibu. Kadhalika katika uzungumzaji wanafunzi walitakiwa kujifunza matamshi bora yaliyo sawa ya wazawa wa lugha ya pili waliyokuwa wakijifunza. 

b) Nadharia ya utabia

Nadharia hii ilitumika sana katika miaka ya hamsini (1950) hadi miaka ya sitini (1960) kule Marekani. Baadhi ya vipengele vya nadharia hii vingali vinatumika mpaka leo. Nadharia hii imejengwa katika misingi ya nadharia ya Saikolojia iitwayo Utabia.

Wafuasi wa nadharia ya utabia walidhamiria kueleza namna tabia inavyojengwa. Waliamini kuwa tabia itadumu ikiwa itaigwa, itarudiwarudiwa, na kutuzwa, lakini tabia isiyorudiwa na isiyotuzwa hufifia.

Kwa hivyo walisisitiza ujifunzaji wa lugha ni sawa na ujifunzaji wa tabia yoyote ile ya binadamu,kama vile kuendesha baiskeli, kuogelea na kadhalika.Kwa hivyo walipendekeza mambo yafuatayo katika ufundishaji wa lugha:

i) Kukariri na kurudiarudia matamshi mazuri ya vipande vya mazungumzo , miundo ya sentensi      n.k

ii) Vipengele vya lugha vifundishwe kwa njia ya kusikiliza na kuongea kwanza kabla ya kuandikwa.

iii) Ufundishaji wa sarufi na vipengele vingine vya lugha usifanywe kwa kuchambua vipengele vya lugha. Mwanzoni wanafunzi wakariri na kurudia na kuiga vipengele hivyo kabla ya kuvizoea.

iv) Jukumu la mwanafunzi ni kufuata maagizo, ilhali lile la mwalimu ni kiongozi wa kila tukio darasani

 

c) Nadharia ya mawasiliano

Nadharia ya mawasiliano ilishika kasi na kupanuka nchini Uingereza katika miaka ya 1970. Lengo kuu la nadharia hii ni kukuza uwezo wa kuwasiliana, lakini siyo kukuza ujuzi wa miundo au vipengele vya lugha tu. Inakusudiwa kukidhi matakwa ya wale wanaojifunza lugha ya pili katika mawasiliano. Mawasiliano yanahusu mambo mengi kama vile, kusababisha mambo fulani yafanyike , kuboresha mahusiano kati ya watu, na kuonyesha hisia za watu na ubunifu wao. Kadhalika, nadharia hii inakusudiwa kuimarisha mbinu za ufundishaji ambazo zitasisitiza uhusiano uliopo kati ya miundo ya lugha mawasiliano.

Nadharia ya mawasiliano ina mihimili ifuatayo.

I.           Maana ya miundo husisitizwa kwani lengo kubwa la nadharia hii ni mawasiliano. Kwa mujibu wa nadharia hii, madhumuni makuu ya lugha ni kuwasiliana, kwani lugha ni mfumo wa kueleza maana.

II.            Vipashio muhimu vya lugha siyo vile vya kisarufi na kimuundo tu, lakini pia vile vya kimawasiliano.

III.            Malumbano (tamthilia fupi) zilitumiwa kufundishia huwa hazikaririwi.

IV.            Muktadha hupewa nafasi muhimu katika ufundishaji. Kwa mfano, maneno mapya au miundo fulani ya kisarufi huwekwa katika muktadha wa mawasiliano, kama vile katika sentensi, mazungumzo na makala.

V.            Drili zinafanywa lakini siyo za lazima kwa mujibu wa nadharia hii

VI.            Matamshi yanayoeleweka na watu wengi katika mazungumzo ndiyo lengo kuu.  Lengo siyo matamshi yanayofanana na yale ya wazawa wa lugha.

VII.            Kanuni za kisarufi na mbinu nyinginezo zinatumiwa inapoonekana kuwa ni lazima.

VIII.            Wanafunzi wanaweza kuzungumza kuanzia siku ya kwanza.

IX.            Lugha ya kwanza na tafsiri zinaweza kutumiwa ikiwa hapana budi, pale matumizi yake yanaposaidia ufafanuzi wa jambo.

 

    X.            Kusoma na kuandika kunaweza kuanza katika siku za mwanzo ikiwa ni muhimu.

XI.            Matumizi ya lugha kwa wingi darasani hupendekezwa kwani nadharia hii husisitiza kuwa mtu hujifunza lugha vizuri kwa kuitumia

XII.            Jukumu muhimu la ujifunzaji wa lugha ni mawasiliano yanayofaa katika muktadha.

 

Nadharia ya mawasiliano inapendekeza ufundishaji ambao unatumia shughuli zinazoedeleza mawasiliano. Hii ni kwa sababu wafuasi wa nadharia hii wanaamini kuwa ujifunzaji wa lugha huendelezwa na vitendo au shughuli zinazoendeleza mawasiliano badala ya ukaririshaji wa miundo. Vitendo kama vile ulinganishaji wa picha, maelezo yanayohusu ramani, maelezo ya ufanyaji wa shughuli fulani kwa mfano, kupika chakula fulani, kuonyesha njia, mazungumzo ya vikundi, tamthilia fupi, uingizaji, michezo, mijadala na usomaji wa magazeti hupendekezwa darasani. Katika darasa la aina hii, mwalimu huchukuliwa kama mratibu wa shughuli hiyo. Kazi yake muhimu huwa ni kuwezesha mawasiliano kuwapo kati ya wanafunzi darasani. Mwalimu pia huwapa wanafunzi ushauri ufaao.

Ni vizuri kutaja kwamba darasa linalotumia nadharia ya mawasiliano hushirikisha wanafunzi sana katika mawasiliano. Mwalimu hasemi yote na kutenda yoye. Jukumu lake huwa limebanwa kidogo. Wanafunzi huhimizwa kufanya mengi darasani.

 

 

 

 

 

 

Eleza umuhimu wa safu mbalimbali za ratiba. 

Ratiba ya kufundishia Kiswahili iko na safu mbalimbali. Safu hizo huwa na umuhimu mkubwa kwa mwalimu wa Kiswahili. Zifuatazo ni safu za ratiba ya kufundishia Kiswahili na umuhimu wake:-

(i)                 Madhumuni ya muhula

Maazimio ya kazi inafaa yatayarishwe kwa kuzingatia mfuatano wa mihula, kila muhula ukiwa na maazimio yake. Kwa hivyo unapotayarisha kazi ya muhula ni lazima uonyeshe maazimio yanayohusika ni ya muhula gani. Pamoja na hayo, kila muhula inafaa ufafanue madhumuni ya ujumla ambayo unatarajia kutimiza katika muhula unaohusika. Ni kutokana na madhumuni hayo ndipo baadaye unapoweza kupata madhumuni maalum ya vipindi

(ii)               Mwezi

Kuhusu mwezi, unachohitaji kutaja ni mwezi wa kufundishia. Kwa mfano, kama

ni muhula wa kwanza, mwezi unaweza kuwa wa kwanza (Januari), wa pili (Februari), au

wa tatu (Machi).

(iii)             Juma / Wiki

Kwa sababu mwezi wenyewe hugawanyika katika majuma/ wiki, inafaa

pia kuonyesha ni wiki gani katika mwezi ambapo unapanga kufundisha jambo fulani

(iv)             Kipindi.

Ni vizuri pia uonyeshe ni kipindi cha ngapi wiki hiyo. Kwa hivyo kabla ya kutayarisha

maazimio ya kazi ni lazima uchunguze katika ratiba ya masomo ya shule ili ujue idadi ya

vipindi ambavyo unatarajiwa kufundisha kila wiki katika somo lako. Kwa kawaida

vipindi vya Kiswahili huwa ni vitano kila wiki lakini vinaweza vikawa vingi au vichache

zaidi kulingana na mpango wa shule.

 

 

(v)               Mada / Yaliyomo

Mada ni kiini cha somo au funzo muhimu katika kipindi fulani. Kwa mfano, mada

inaweza kuwa: Insha ya methali. Kama hiyo ndiyo mada ya kipindi chako inakubidi pia

ujiulize kile ambacho unatarajia wanafunzi wafanye kuhusu mada inayohusika. Tuseme,

kwa mfano, kwamba unataka wanafunzi wako waandike insha inayobainisha ukweli wa

methali fulani. Ni lazima ueleze jambo hili kwa kauli maalum; na unapofanya hivyo

utakuwa unatoa lengo la kipindi.

(vi)             Madhumuni / Malengo ya kipindi

Baada ya kuteua mada  ya kipindi ni lazima  uteue kile ambacho unatarajia wanafunzi wafanye kuhusu mada huska.Pamoja na kufafanua malengo / madhumuni maalum ya kipindi ni lazima

upendekeze kazi ya kushirikisha wanafunzi wakati kipindi cha somo kinapoendelea.

(vii)           Mazoezi / Kazi ya wanafunzi

Kazi ya kushirikisha wanafunzi ni lazima ihusiane na mada inayohusika pamoja na malengo

yaliyowekwa. Kazi yenyewe inalenga kuchangia katika utekelezaji wa malengo

yaliyofafanuliwa. Wakati mwingine kazi hii hujulikana kama enabling objectives kwa

Kingereza. Ni kupitia mazoezi haya / kazi hii ndipo malengo yanayotarajiwa kufikiwa

yanapoweza kutimizwa.

(viii)         Vifaa / Marejeleo

Hali kadhalika, unapotayarisha maazimio ya kazi unahitaji vifaa ambavyo huenda

ukavitumia wakati wa kufundisha. Hivi navyo vimetengewa nafasi yake katika muundo

wa maazimio ya kazi.

 

(ix) Maoni

Sehemu nyingine muhimu ni ile ya maoni. Katika sehemu ya maoni unapaswa

kutoa maelezo kuhusu jinsi mada fulani ilivyofundishwa. Unaeleza jambo lo lote ambalo

huenda lilitokea na kuathiri utekelezaji wa mpango wako. Kila unapoandika maoni

kuhusu kipindi cha somo huwa unajitathimini utendaji kazi wako. Maoni unayoandika

yanalenga kukusaidia unapojiandaa kwa vipindi vitakavyofuata baadaye. Ikiwa kwa

mfano, kipindi chako kilikuwa cha kufana, inafaa ueleze mambo ambayo yalichangia

kukifanikisha. Hali kadhalika, ikiwa kipindi hakikufaulu kama ilivyotarajiwa inafaa

uonyeshe hatua unazopanga kuchukua ili kurekebisha hali. Kwa hivyo, ni lazima utilie

maanani sana mambo unayoandika kama maoni

 

Hata hivyo, kuna aina nyengine yabratiba ambayo ni muhimu kuiangazia.

Ratiba ni orodha ya mpangilio wa namna mambo yatakavyofuatana katika shughuli fulani. Lengo lake ni kuhakikisha wakati unatumiwa vizuri ili mambo fulani yasije yakakosa kutendwa kutokana na upungufu wa wakati.

Ratiba hutumika katika sherehe, mikutano, mazishi, hafla, tamasha, n.k

Sehemu za Ratiba

 

Kichwa

    Kichwa cha ratiba hutaja mambo yafuatayo:

        Shughuli yenyewe – Taja jina la tukio ambalo unaandalia ratiba. Kwa mfano Harusi ya Bwana na Bi Arusi, Siku ya Zawadi

        Tarehe ya shughuli – je shughuli hiyo itafanyika lini?

        Mahali- Taja mahali ambapo shughuli hiyo itafanyikia. kwa mfano katika uwanja wa michezo wa Kasarani, kanisa la St. Mtakatifu

    Mfano wa kichwa cha ratiba:

        Ratiba ya Hafla ya Ukimwi katika Bustani la Uhuru tarehe tano Januari.

        Ratiba ya Mazishi ya Dkt. Marehemu tarehe 20/12/1923 Kijijini Vikwazoni

 

 

 

Mwili

    Mwili wa ratiba hujumuisha mambo mbalimbali yatakayofanyika katika mpangilio maalum, saa mbalimbali. Ni vizuri kuzingatia vipengele vifuatavyo:

        Saa – Onyesha saa ambazo tukio limepangiwa kuanza hadi linapotakiwa kumalizika

        Mahali – Ikiwa shughuli tofauti zinafanyika katika mahali mbalimbali kama vile vyumba tofauti, inapaswa hutaje mahali ambapo kila jambo litafanyikia.

        Wahusika – Taja mtu au watu waliopewa wajibu wa kutekeleza jambo fulani. Hii huwasaidia kujitayarisha ipasavyo.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

REFERENCE

Musau P.M. & Chacha L.M. (2001): Mbinu sa Kisasa za Kufundisha Kiswahili,

Kenya Literature Bureau.

5. Gerald Njagi Matti (2002), Introduction to The Study of Literature, Institute of

Open Learning, Kenyatta University.

6. K. W. Wamitilia (2002), Uhakiki wa Fasihi Msingi na Vipengele Vyake. Phoenix

Publishers Ltd

Comments

Popular posts from this blog

NI SABABU ZIPI ZINAZOFANYA MZUNGUMZAJI WA LUGHA KUFANYA MAKOSA YA KISARUFI NA KIMATAMSHI NA KIMANTIKI KATIKA LUGHA?

Methali, Vitendawili, nahau, misemo,

NADHARIA ZINAZOELEZEA CHIMBUKO LA FASIHI SIMULIZI/MASIMULIZI