NI SABABU ZIPI ZINAZOFANYA MZUNGUMZAJI WA LUGHA KUFANYA MAKOSA YA KISARUFI NA KIMATAMSHI NA KIMANTIKI KATIKA LUGHA?

NI SABABU ZIPI ZINAZOFANYA MZUNGUMZAJI WA LUGHA KUFANYA MAKOSA YA KISARUFI NA KIMATAMSHI NA KIMANTIKI KATIKA LUGHA?


Athari ya lugha ya kwanza,kuzungumza kwa haraka,kujumlisha kanuni zinazotawala lugha zingine
Athari ya lugha ya Kwanza
Hali ya kiafya kama vile ugongwa
Kutoelewa sheria za lugha hiyo
Kuongea kwa haraka
1kutoelewa lugha kikamilifu
2.kukosa istilahi rasmi
3.Athari ya lugha nyingine mf lugha mama
4.Maumbile mf kithembe
Daaa!unanikumbusha nikisomea mitihani ya Prof.Riro matinde
Mazingira. Mfano maeneo ya mipakani.
Athari za lugha ya kwanza.
Ulemavu (mtu aliye na kithembe)
Kuteleza kwa ulimi
Kutokuelewa lugha fasa ya kiswahili, au kutoishi kwenye mazingira ya waswahili na kujuwa jinsi ya kutamka herufi.
wanafunzi wanaojifunza lugha ya Kiswahili kama lugha yao ya pili, zimejikita zaidi
katika matatizo ya kijumla, nyingi ni katika kiwango cha kimofolojia, kifonolojia na
kimofosintaksia
Aidha Kiswahili ni lugha iliyo na majukumu mengi kama tulivyoeleza awali. Zaidi ya
kuwa ni lugha inayotumiwa katika mawanda mapana kama vile siasa, utawala na
biashara miongoni mwa mengine, pia ni lugha inayowaunganisha wanajamii
mbalimbali kwa kuwa hutumiwa na wazungumzaji ambao lugha zao za kwanza ni
tofauti.Uchanganuzi Makosa ni muhimu kwa sababu humwezesha mtafiti kujua jinsi watu
hujifunza lugha na mikakati wanayotumia katika harakati za kutambua lugha lengwa
kutokana na L1. Wanafunzi hutumia lugha yao ya mama ili kuunda mifumo
ya lugha legwa. Kwa kufanya hivi, sio kosa bali ni njia ambayo wanafunzi
wengi hutumia kuunda mifumo ya lugha. Tofauti iliyopo baina ya kujifunza
lugha ya kwanza na ya pili ni kuwa ujifunzaji wa lugha ya pili huathirika na
lugha ambayo tayari mwanafunzi anaijua. Kuathirika huku ndiko kunaitwa
uhamishaji wa lugha. Uhamishaji lugha waweza kutokana na lugha ya
kwanza, pili au tatu na hutokea katika viwango tofauti k.v. sarufi, matamshi,
msamiati, diskosi, n.k.
2. Mikakati ya ufundishaji mbaya wa lugha ya pili kutokana na uelewa mbaya
wa mwalimu, wa umilisi wa kiisimu pamoja na mbinu mbalimbali za
ufundishaji wa lugha ya pili. Mwanafunzi hujifunza lugha kwa kusikia
mwalimu wake anavyozungumza. Mwanafunzi anaposikia matamshi mabaya
kutoka kwa mwalimu, naye hufanya makosa hayo bila kujua. Hii ni kwa
sababu mwalimu ni mzungumzaji wa lugha ya kwanza na kwa hivyo katika
kufundisha yeye hufanya makosa.
3. Ujumlishaji mno - Kanuni za lugha lengwa hujumlishwa.Wanafunzi hutumia
kanuni za lugha ya pili namna ambavyo wazawa wa lugha hii hawawezi
kutumia. Watafiti huamini kuwa miundo hii ya lugha hutokana na ujuzi
alionao mwanafunzi katika akili yake. Mwanafunzi hujumuisha sifa za lugha
pale ambapo sifa za lugha anayojua zinakaribiana na zile za lugha
anayojifunza. Hii husababisha ucheleweshaji wa uelewa wa sifa tofauti.Mwanafunzi anaweza kukataa kujifunza kanuni zilizo tofauti na lugha yake ya
kwanza.
4. Mikakati ya kujifunza L2. Wanafunzi husahilisha sarufi ya L2 ili kufikia
uamilifu mpana wa mawasiliano. Mwanafunzi anapojifunza lugha hutaka
kurahisisha matamshi katika mawasiliano.
5. Mkakati wa kuwasiliana katika L2. Mawasiliano katika L2 hutokana na njia
mahususi ambazo watu hujifunza ili kuweza kuwasiliana ili kukabiliana na
upungufu wa L2. Mtazamo huu uliibuka kukidhi upungufu wa uchanganuzi linganuzi uliotumiwa na
wanaisimu kutofautisha lugha ya kwanza na ya pili ya mwanafunzi ili kukisia makosa.
Uchanganuzi makosa ni mbinu itumiwayo kuthibitisha makosa yanayopatikana katika lugha
ya mwanafunzi. Walimu wa lugha wanaowasikiliza wanafunzi wao wakizungumza hutambua
makosa. Ukweli ni kuwa kila mtu hufanya makosa anapoongea hata walimu na wazawa wa
lugha hufanya makosa. Wazawa wa lugha hawafuati kanuni za sarufi zilizoandikwa vitabuni Tunapowasikiza wanafunzi wakizungumza tunafahamu makosa wayafanyayo. Kwa sababu
hii ni vyema kujiuliza kile mzungumzaji alikusudia kukisema na angekisema vipi.
Kusahihisha makosa haya sio jambo rahisi kwa sababu kuna zaidi ya njia moja ya kufanya
hivyo. Kusahihisha makosa kunategemea kile msikilizaji anafikiri mzungumzaji alikusudia
kukisema na kosa lenyewe. Ni vyema kufikiri namna nyingi tofauti za kusahihisha makosa.
Kwa sababu huna uhakika wa kilichokusudiwa, mwache mwanafunzi akusaidie kuamua
sahihisho sahihi.
Kufafanua makosa haya, kwataka kujua kisababishi. Makosa yanaweza kutokana na
kuhamisha kanuni au ruwaza za lugha ya kwanza. Makosa mengine yanaweza kusababishwa
na jinsi mwalimu au vitabu vya kaida vinavyoeleza kanuni fulani. Au inaweza kuwa mikakati
ya mawasiliano anayotumia mwanafunzi hata kama anajua kanuni anazotumia sio sahihi.
Utafiti huu si linganishi kwa sababu hatujalinganisha lugha mbili ili kutambua makosa. Kwa
hivyo Mtazamo wa Uchanganuzi Linganishi hautafaa katika utafiti wetu. Aidha, utendaji wa
wanafunzi katika uandishi wa insha hauwezi kuchunguzwa kwa kutumia mtazamo huu.
Katika utafiti huu tumetumia mitazamo miwili nayo ni Uchanganuzi Makosa na Lugha
Kadirifu kwa kuwa ndiyo hutilia maanani makosa yote yanayosababishwa na mambo
mengine mbali na athari za L1.
Baadhi ya makosa yanasababishwa na lugha ya kwanza, Kiingereza na Sheng.
Aidha, ujumlishaji mno ulidhihirika kusababisha makosa ya kimofosintaksia. Utafiti wetu ni
tofauti kwani umelenga kundi mahususi.
Athari za kimofonolojia za Kiolusuba katika matumizi ya Kiswahili Sanifu kama lugha ya pili. Utafiti huu ulidhihirisha kuwepo kwa tofauti kubwa
baina ya mifumo ya fonimu za Kiswahili na Kiolusuba ambayo huathiri matumizi ya
Kiswahili. Aidha utafiti huu umelinganisha miundo ya silabi za Kiolusuba na za Kiswahili
ambapo amepata ni tofauti. Tofauti hii amepata inachangia katika athari hiyo. Utafiti huu ni
tofauti na wetu kwani haukushughulikia kiwango cha kisintaksia na hivyo hakujishughulisha
na miundo ya sentensi na upatanisho wa kisarufi.
Ni muhimu kuwa  mwangalifu wakati wa kuongeza na kuondoa irabu kwa baadhi ya maneno. Kwa mujibu wa misingi ya uandishi wa maneno ya Kiswahili, inafahamika kuwa maneno mengi ya Kiswahili huishia kwa irabu. Hata hivyo yako  maneno  machache sana ya Kiswahili ambayo hayaishii kwa irabu kama vile mathalan, takriban, hususan. Maneno yafuatayo yanaishia kwa irabu kama  maalumu, salamu, mwalimu, mtaalamu, nk. Nikumbushe pia kwamba neno waalimu linatakiwa kuandikwa walimu na pia neno umaarufu lisiandikwe umarufu. Neno neema lisiandikwe  nema, rehema siyo rehma, azima badala ya azma, riziki badala ya riski, rutuba badala ya rutba.Jambo muhimu la kuzingatia ni kuepuka kuongeza viambishi  kama ma mbele ya maneno  hasa yale yenye asili ya kigeni. Hili ni tatizo linalojitokeza katika mazungumzo na hotuba za viongozi ambapo baada ya kutolewa huandikwa na waandishi  bila kuhaririwa kwa makini ili kuwa Kiswahili fasaha. Waandishi wanadhani kuwa kile kinachozungumzwa na kiongozi wa chama au serikali ni sahihi na hakiwezi kurekebishwa. Hili ni kosa.Ni lazima kuihariri kazi ya kiongozi kama vile hotuba bila kubadilisha maudhui yake. Hii ni hatua katika uandishi ambapo lengo ni kutoa taarifa sahihi kwa lugha fasaha. Lengo ni kutekeleza wajibu wa kazi yako kwa mujibu wa taaluma ya uandishi. Ieleweke kuwa kuhariri kazi ya uandishi si kubadili maana bali ni kuiweka lugha katika misingi yake ya kisarufi, kimantiki na kisementiki.Kwa mfano, wako wanasiasa na pia wataalamu wa fani mbalimbali wanayatumia maneno kadhaa ya Kiswahili ama kwa kuongeza au kupunguza viambishi vya awali. Kwa mfano yako maneno kama mapungufu badala ya upungufu, maamuzi badala ya uamuzi, mashirikiano badala ya ushirikiano, mashule badala ya shule, mahospitali badala ya hospitali, mabenki badala ya benki, manunuzi badala ya ununuzi.Kwa maana hiyo, mwandishi au mtangazaji anapokutana na hali kama hiyo, kwa mujibu wa maadili ya kazi yake anapaswa kufanya marekebisho bila kujali hadhi ya mzungumzaji au mwandishi.Yafaa tuzingatie kwamba baadhi ya makosa haya yanaambatana na tahajia ambapo Kiswahili ni lugha ya kifonetiki yaani inatamkwa vile inavyoandikwa isipokuwa kwa baadhi ya maneno machache tu.Baadhi ya makosa yanayojitokeza yanatokana na athari ya lugha za asili na pia lugha za kigeni. Mwandishi na mtangazaji anatakiwa kuwa makini sana ili kumfanya aeleweke na wasikilizaji wake. Athari ya lugha ya asili inasababisha waandishi washindwe kutofautisha ya vitamkwa viwili ambavyo ni /dh/ na /th/. Lugha nyingi za asili hutufanya tushindwe kumudu Kiswahili sanifu na fasaha. Tatizo hili lipo na suluhu ni kuwasomesha walimu wetu katika taaluma ya isimu, hasa fonolojia.Matokeo yake yatakuwa ni mafanikio makubwa katika kukamilisha lengo
MAKOSA YA KISARUFI NA KIMANTIKI KATIKA LUGHA
Pale lugha inapotumika tofauti na malengo hupoteza lengo na madhumuni ya mzungumzaji kwa msikilizaji wake. Upotoshaji huu hujitokeza katika sarufi au mantiki.
MAKOSA YA KISARUFI
Kila lugha ina kanuni na taratibu ambazo hutawala katika matumizi ya lugha ili watu waweze kuelewana kanuni hizo zinapovunjwa au kukiukwa huweza kusababisha makosa kujitokeza na upotovu katika lugha. Makosa ya kisarufi yanaweza kugawanyika katika sehemu zifuatazo:-
Makosa ya kimsamiati
Makosa ya kimuundo
Makosa ya matamshi
Kuongeza vitamkwa au viambishi
Kuacha maneno
Makosa ya tafsiri sisi
Makosa ya kimsamiati
Watumiaji wa lugha huchanganya masamiati wakati wa kuzungumza au kuandika. Watu hutumia msamiati usiolingana na msamiati usiolinga na maana iliyokusudia
Mfano:- Nona na nenepa
Wengi husema siku hizi umenona sana.
Badala ya kusema, Siku hizi umenenepa sana.
mazingira na mazingara
Watu husema Mazingara yameharibiwa sana siku hizi.Badala ya kusema Mazingira yameharibiwa sana siku hizi.Ajali na ajili
Watu husema Amefariki wa ajili ya gari.
badala ya kusema Amefariki kwa ajali ya gari.
Wakilisha na wasilisha
Watu husema, Waziri wa fedha atawakilisha bajeti ya mwaka kesho.
Badala ya kusema Waziri wa fedha atawasilisha bajeti ya mwaka kesho.
Makosa ya kimuundo
Kwa kawaida sentensi za kiswahili huanza na nomino ya mtenda au mtendwa.
Mfano:- mtoto mpole anacheza
Mzungumzaji asiye fuata kanuni husema Mpole mtoto anacheza.
Kalamu yangu imeibwa.
badala ya kusema kalamu yangu imeibiwa.
Makosa ya kimatamshi
Watu wengi hushindwa kutamka baadhi ya sauti za kiswahili wakati mwingine huchanganya na kubadili sauti hizo Mfano Wakurya hutumia ’r’ badala ya ’l’
Nenda karare
badala ya kusema nenda kalale
Wandali hutumia ’s’ badala ya ’z’ na ’dh’ na ’th’
mfano selasini
badala ya thelathini
Sahabu
badala ya dhahabu
Samani
Badala ya zamani
Makosa haya mara nyingi yanatokana na athari ya lugha mama. Kwa kuwa lugha ya kiswahili ni lugha ya pili kwa wazungumzaji wengi. Hivyo lugha ya kwanza huwa na athari kubwa kwa mzungumzaji wa wa lugha ya pili.
Kosa la kuongeza vitamkwa
Baadhi ya wazungumzaji huongeza vitamkwa mahari pasipo hitajika na hivyo kuharibu lugha.
Mfano. Nendaga
badala ya nenda
Mashule
badala ya shule
Huwaga anapenda fujo
badala ya huwa anapenda fujo
Kosa la kuacha maneno
Watumia lugha huweza kuacha maneno katika sentensi na bado wakafikiri wanatoa ujumbe uleule uliokusudiwa.
mfano, Watu husema Juma ameondoka kazini akiwa na maana kuwa Juma ameondoka kwenda kazini lakini sahihi ni kuwa Ametoka kazini.
Alfredi amerudi kazini akiwa na maana kuwa Afredi ametoka kazini.
Kwa mzungumzaji anatoa maana ambayo ni kinyume kabisa na ile maana aliyo kusudia kusema. Ambapo anakusudia kuuliza kama Alfredi amekwenda tena kazini.
Makosa ya tafsiri sisisi
Tafsiri sisisi ni tafsiri ya neno kwa neno. Tafsiri hii inapofanywa huleta matatizo ya kisarufi katika lugha
mfano. Kimbizwa hospitali
She runed to hospital
badala ya kusema amepelekwa hospitali
At the end of the day
Mwisho wa siku.
Badala ya kusema hatimaye.
MAKOSA YA KIMANTIKI
Mantiki ni utaratibu mzuri wa kufikiri. Makosa ya kimantiki ni yale yanayoonesha kukosekana kwa utaratibu wa fikra. Nimakosa yanatokana na upotovu wa mawazo ya mzungumzaji.
Mfano; watu wengi husikika wakiema hivi: Usimwage kuku kwenye mchele mwingi
Badala ya usimwage mchele kwenye kuku wengi
Nyumba imeingia nyoka
Badala ya kusema Nyoka ameingia ndani ya nyumba
Chai imeingia nzi
Badala ya kusema Nzi ameingia kwenye chai.
KUSAHIHISHA MAKOSA
Katika lugha yeyote ile makossa ya kawaida yataendelea kuwepo kama ilivyo katika lugha ya Kiswahili, kwa hiyo hatuna budi kujitahidi kusahihisha na kuzuia makosa hayo.
Watumiaji wa lugha inawabidi kuhakikisha makosa ya kisarufi na kimantiki katika msamiati, matamshi, muundo na maana hayaendelei kujitokeza kwenye mazungumzo, barua, shuleni na hata kwenye vyombo vya habari kama vile Magazeti, redio na televisheni.
Jambo la muhimu ni lazima jitihada za marekebisho ya kisarufi na kimantiki zitiliwe mkazo tangu kiwango cha elimu ya shule ya msingi, sekondari na vyuoni hadi vyuo vikuu.
Mara kadhaa makosa ya kimsamiati yamekuwa yakisababishwa na vyombo vya habari kwa hiyo ni muhimu somo la matumizi wa lugha ya Kiswahili lizingatiwe vyema katika vyombo vyote vya habari ili kuepusha upotoshaji wa lugha.
Kwa sababu hiyo kamusi inabaki kuwa kitabu muhimu sana kwa sababu huwa na orodha ya maneno mbalimbali yanayotumiwa na wazungumzaji wa lugha na maana zake.

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

Methali, Vitendawili, nahau, misemo,

NADHARIA ZINAZOELEZEA CHIMBUKO LA FASIHI SIMULIZI/MASIMULIZI